Kiswahili kina mameno machache,
tafsiri ya ‘obey’ na ‘submit’ yote ni utii kwa Kiswahili, lakini kwa
uhalisia ‘submit’ ni zaidi ya ‘obey’.’Submit’ ni kukubali kwa
unyenyekevu kuwa chini ya mamlaka fulani, kuiamini hiyo mamlaka na bila
kujaribu kuwa juu yake, na ‘obey’ ni kufanya kile unachoambiwa na
mamlaka iliyo juu yako. Hivyo utii wa submit ni zaidi ya utii wa obey.
Ni kuamua kuwa chini ya mamlaka hiyo na sio kusubiri kuambiwa kitu ndipo
utii. Utii wa mke kwa mume ni ‘submit’, kuamua kuwa chini ya uongozi wa
mume wako, kuuheshimu na kumwamini kuwa anaweza kuwaongoza bila kutaka
kuingilia nafasi yake kama kiongozi.
Jambo hili limekuwa ni gumu sana
kwa wanawake wengi hasa wale ambao wana kipato, wlimu, huduma au nafasi
katika jamii zaidi ya waume zao. Biblia inawataka wake wote kuwatii
waume zao bila kujali hali zao wala nafasi zao au kama wameokoka ama la.
Waefeso 5:22-24 Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu. Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha kanisa; naye ni mwokozi wa mwili. Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo na wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.
Mistari hii katika biblia
inatuonyesha jinsi gani inavyotupasa kuwatii waume zetu. Paulo
amefananisha utii huu na utii wa kanisa kwa Kristo, utii wa kuamua toka
moyoni kunakosukumwa na upendo na wala sio utii wa kulazimishwa. Ni utii
katika kila jambo, dogo hadi kubwa kama vile kanisa linavyomtii Bwana
Yesu. Ila tunapewa angalizo, “kama ipendezavyo katika Bwana”. Hivyo
hatupaswi kutii pale ambapo tunaelekezwa kutenda kinyume na mapenzi ya
Mungu.
Kolosai 3:18 Ninyi wake, watiini waume zenu, kama ipendezavyo katika Bwana.
Unaweza kusema kuwa mume wako
hajaokoka na wewe umeokoka hivyo ni vipi sasa utajiweka chini ya uongozi
wake? Biblia inalojibu kama tunavyoona hapa katika mistari hii
ifuatayo.
1 Petro 3:1-2 Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno;
Kumbe utii wako kwa mume wako
kunaweza kumfanya akaokoka bila hata mahubiri ya maneno mengi. Kutii sio
utumwa, ni kuitambua nafasi ya mume wako na nafasi yako kama mke kwenye
ndoa yenu. Unapoitambua nafasi ambayo Mungu amekupa utashangaa utii
unakuja bila hata kujisukuma. Wewe ndiwe mlezi wa familia, mfariji wao,
muangalizi, mfundishaji watoto na mengine mengi. Soma Mithali 31:11-31
Katika biblia tunaona jinsi Sarah
alivyokuwa mtii kwa mume wake Abrahamu. Mume wake alipomuambia kwamba
Mungu amesema watoke katika nchi yao na waende katika nchi
atakayowaambia wasipopajua wao, sarah alimtii bila kubishana naye.
Alikuwa tayari kuondoka mahali alipopazoea na kuenda na mume wake
asipopajua kwa sababu alimuamini Mume wake na kuwa tayari kuongozwa
naye. Mwanzo 12:1-9
Mume anajukumu kubwa sana la
kumpenda mke wake kama Kristo kwa kanisa, upendo usio na sababu, upendo
wa kujitoa kwa ajili yake, upendo wa kumtanguliza. Mume anapofanya haya
ni rahisi sana kwa mke kumtii bila kuona uzito, ila hata kama mume wako
bado hajafikia kiwango hicho cha upendo, wajibu wako wa kumtii upo pale
pale na hapo utaziona Baraka za Mungu katika ndoa yako.
Ubarikiwe na Bwana Yesu.
Mgalula Y.Joseph
0752601632/0655601632