Thursday, 24 March 2016

HAKIKA KILA NAFSI ITAONJA MAUTI.
IT DOES`NT MATTER HOW RICH ARE YOU
IT DOES`NT MATTER HOW FAMOUS ARE YOU.
Zaburi 118:17... INASOMEKA HIVI. HAUTAKUFA UTAISHI NA KUYASIMULIA MATENDO YA MUNGU.

HAINA MAANA KUWA HATUTAKUFA MIILI YETU, NENO HILI LINAMAANISHA HATUTAKUFA ROHO NA NAFSI ZETU AMBAKO HUKO NDIKO UKAAKO UZIMA WA MILELE NA NI MAKAO YA ROHO MTAKATIFU. ROHO MTAKATIFU HUISHI HUKO ILI KUMFANYA MTU AWE NA UZIMA WA ROHO NA NAFSI YAKE. NAFSI NA ROHO ZIKICHAFUKA KWA MAANA YA KUJITENGA NA UWEPO WA MUNGU NAFSINI MWETU AU KWA LUGHA NYINGINE KUTENDA DHAMBI ROHO MTAKATIFU HUONDOKA NA KUKAA KANDO MAANA TUNAKUWA HATUNA UZIMA WA ROHO NA NAFSI ZETU.

mithali 14:34, “dhambi ni aibu ya watu wo wote” ),lakini msamaha wa MUNGU ukiingia ndani ya mioyo yetu nyuso zetu hazitaona haya milele.

UKISOMA WALAKA WA MTUME PAUL KWA WAFILIPI 1:21 INASOMEKA HIVI
"Kwa maana kwangu mimi kuishi ni Kristo, na kufa ni faida" HII INA MAANA KWAMBA KUISHI KWETU NI KWA MSAADA WA YESU KRISTO NA KUFA NI FAIDA IKIWA TUNAKUFA KATIKA BWANA. SIKILIZA MTUMISHI WA BWANA SOTE TUNAISHI KATIKA ULIMWENGU MMOJA NA DUNIA MOJA. NI LAZIMA TUKUMBUKE KUWA SIKU MOJA TUTAKUFA MIILI YETU LAKINI NAFSI ZETU NA ROHO ZETU ZITAKUWA ZI NGALI HAI. NI JUKUMU LETU MIMI NA WEWE KUHAKIKISHA TUNAISHI MAISHA YA KUMPENDEZA BWANA. LEO HII TU WAZIMA HATUJUI HATMA YA SIKU ZETU TUWAPO DUNIANI. UKIANGALIA PICHA HII HAPA CHINI UTAJIFUNZA KITU KIKUBWA SAANA, NA MTENGENEZA PICHA HUENDA ALIDHANI ANATENGENEZA PICHA KWA KUJIFURAHISHA LAKINI NDIYO UKWELI HALISI.

HIVI FIKIRIA MPENDWA WA BWANA ULIKUWA UKILALA KATIKA KITANDA KIZURI SAANA GHAFLA KUFUMBA NA KUFUMBUA UNAENDA KULALA KATIKA MAVUMBI/MATOPE, HILI NI FUMBO KUBWA SAANA BWANA AMETUPATIA. ULIKUWA UKITEMBELEA GARI LA KIFAHARI KABISA LAKINI KUFUMBA NA KUFUMBUA HAUPO TENA DUNIANI; MUNGU ATUSAIDIE WAPENDWA TUTENDE MEMA TUWAPO DUNIANI.
PICHA HII INATUKUMBUSHA KUWA KUNA SIKU TUTAKUFA NA VYOTE TULIVYONAVYO VITABAKI. HAKUNA ATAKAYEENDA NA MALI ZAKE. KILA KITU KITABAKI DUNIANI. HATMA YA MAISHA YETU IPO MIKONONONI MWA MUNGU MWENYEWE. MUNGU ATUREHEMU NA ATUPE NEEMA YA KUONA HAJA YA KURUDI UWEPONI MWAKE. TU WENYE DHAMBI TUSIOSTAHILI HATA KUTAMKA JINA LAKE MAANA NI TAKATIFU NA VINYWA VYETU NI VICHAFU.
NAWATAKIA PASAKA NJEMA, TUFE NA BWANA NA TUFUFUKE NAYE.
MUNGU AWABARIKI NYOOOOTE.
AMENI.
Mgalula, Y.J.

Friday, 11 March 2016

 
UFAHAMU ULIMWENGU WA ROHO.
Tukiwa hapa duniani, wengi tunaona ulimwengu huu kwa jinsi ya mwili, na mambo mengi yanayoendelea. Wakati mwingine tunaziona na kazi mbalimbali zinazoendelea duniani, na wakati mwingine tunasikia tu, kwa njia ya vyombo vya habari. Maranyingi tumesikia falme zikipigana, na mara nyingine tumesikia habari za mataifa na hata watu mbalimbali wakitafuta maendeleo. Zipo kazi nyingine ambazo hazionekani kwa macho lakini zinafanyika kwa jinsi ya mwili, kwamfano; tunaweza kutumia mtandao wa intaneti, simu, redio na hata vinasa taarifa mbalimbali. Tunaweza kuviongoza vyombo vikubwa kwakutumia kifaa kidogo kama vile vidhibiti vya mbali (remote control). Mambo haya yote hayahitaji imani ili yatokee, maana yamekuwa yetu, bali yanahitaji akili, maarifa na ujuzi.
Kama tunavyouona ulimwengu huu wa mwili, vivyohivyo upo ulimwengu wa kiroho, ambao huwezi kuuongoza kwa jinsi ya mwilini. Huo nao umesheheni kazi nyingi mno ambazo kwa kiasi kikubwa ndio unaoratibu mambo yote yanayotokea kwa jinsi ya rohoni, na yale yanayotokea kwa jinsi ya mwili. Tofauti iliyopo ni kwamba, katika ulimwengu wa roho si kila mtu anaweza kuingia na kufanyanya kazi, zaidi ya hayo ulimwengu wa roho unahitaji imani kama mtaji, ndipo mtu anaweza kufanya kazi (1kor 2:14).
Kama ilivyo kwa ulimwengu wa mwili, vivyohivyo katika ulimwengu wa roho kuna falme, mamlaka, miji, majeshi, malango, ngome, kuta, sheria, na hata vyombo vya maamuzi kama vile; bunge na mahakama. Katika ulimwengu wa roho kuna falme mbili, ambazo ni ufalme wa Mungu na ufalme wa shetani. Hii haimaanishi kuwa shetani anao ufalme unaoweza kushindana na Mungu, bali mwanadamu ndiye anayeshindana na shetani, ili kutetea nafasi aliyopewa na Mungu, kisha akaipoteza.

UFALME WA MUNGU.
Ufalme wa Mungu ulikuwako kabla ya ulimwengu kuwako, hauna mwanzo wala mwisho (Kol 1:17, Mith 8:20-31). Mungu alipoumba mbingu na nchi, alimuumba mwanada kuwa roho inayoishi, akampa mwili kutoka ardhini (Mw 1:26-27, Yoh 3:6, Yoh 1:13, Yoh 4:24, Mwa 2:7, 3:19). Tofauti na viumbe vyote vilivyo katika ulimwengu wa roho, roho ya mwanadamu iliwekwa ndani ya mwili, uliofanyika kutoka udongoni. Hivyo mwanadamu alipewa nafasi ya kuishi katika ulimwengu wa roho, na katika ulimwengu wa mwili kwa wakati mmoja.
Ili kumfanya mwanadamu kuwa mtawala pekee katika dunia, Mungu alitengeneza sheria katika ulimwengu wa roho (Ayub 38:33, Zab 8:5-6). Sheria hizi ndizo zilizoitofautisha nafasi ya mwanadamu katika ulimwengu wa roho, ukilinganisha na malaika na viumbe vingine vyote vilivyopo katika ulimwengu wa roho. Mwanadamu alishirikishwa mamlaka ya Mungu, kwa kupewa nafasi ya kutawala dunia. Hivyo mwanadamu alikuwa, anawakilisha ufalme wa Mungu duniani. Yesu alipokuja duniani, alikuja kutukomboa, na kuturudishia nafasi tuliyokuwa tumepoteza katika ulimwengu wa roho.
UHALISIA WA ULIMWENGU WA ROHO.
Kabla hatujaendelea sana na somo hili, ninapenda ufahamu kuwa, tunapozungumza kuhusu ulimwengu wa roho, tunaweza kugawanya katika makundi makubwa mawili. Kundi la kwanza tutazungumzia kuhusu Mbinguni, ambako Mungu ndiye mfalme pekee wala hakuna mwingine. Kundi la pili tutazungumzia, eneo linalotawala dunia kwa jinsi ya rohoni, maana yake ulimwengu wa roho unaotawala dunia. Katika kitabu cha zaburi anasema, “Mbingu ni mbingu za Bwana, Bali nchi amewapa wanadamu” (Zaburi 115:16).

Dunia inasehemu mbili, ambazo ni ulimwengu wa roho, na ulimwengu wa mwili (Mwanz 1:1-2). Kumbuka hapa hatuzungumzii habari ya anga na ardhi, bali tunazungumza habari ya ulimwengu wa roho unaotawala dunia, na ulimwengu wa mwili. Hapa duniani katika ulimwengu wa roho zipo falme mbili, ambazo ni ufalme wa nuru (Mungu), na ufalme wa giza (shetani). Mungu alimrudisha mwanadamu kwenye nafasi yake, kwa njia ya kifo cha Bwana Yesu pale msalabani. Isaya alitabiri akisema; “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, tumepewa mtoto mwanamume; na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa Jina Lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.7 Maongeo ya enzi yake na amani Hayatakuwa na mwisho kamwe, Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele. Wivu wa Bwana wa majeshi ndio utakaotenda hayo.

Katika mistari tuliyoisoma hapo juu, ninaweka mkazo katika maneno yafuatayo, angalia neno ‘kwaajili yetu’. Hii inamaanisha kuwa Yesu alizaliwa kama mfalme duniani kwaajili yetu. Mabegani mwake alibeba uweza wa kifalme, ili kuleta ufalme usiokoma duniani. Ninachotaka udake hapa ni kwamba, Yesu alikuja kuuleta ufalme wa Mungu duniani, lakini si katika ulimwengu wa mwili, bali katika ulimwengu wa roho. Hivyo Yesu alizaliwa kama mfalme wa dunia katika ulimwengu wa roho, ndiyo maana anatajwa kuketi katika kiti cha enzi cha daudi. Angalia maneno ya Yesu katika injiri ya Yohana 18:36, anasema; “Yesu akajibu, Ufalme wangu sio wa ulimwengu huu. Kama ufalme wangu ungekuwa wa ulimwengu huu, watumishi wangu wangenipigania, nisije nikatiwa mikononi mwa Wayahudi. Lakini ufalme wangu sio wa hapa.37 Basi Pilato akamwambia, Wewe u mfalme basi? Yesu akajibu, Wewe wasema, kwa kuwa mimi ni mfalme. Mimi nimezaliwa kwa ajili ya haya, na kwa ajili ya haya mimi nalikuja ulimwenguni, ili niishuhudie kweli. Kila aliye wa hiyo kweli hunisikia sauti yangu”.


Ndugu mpendwa, sasa unaelewa kuwa Yesu alikuja ulimwenguni, kuleta ufalme wa Mungu, lakini si kwa jinsi ya mwili, bali katika ulimwengu wa roho (Mwanz 3:15, 49:10, Kumb 18:15, Dan 2:44-45,). Shida haikuwa Mbinguni katika ulimwengu wa roho, bali shida ilitokea duniani katika ulimwengu wa roho. Hivyo Mungu alipoteza nafasi yake duniani kama mfalme, kwasababu mamlaka katika ulimwengu wa roho duniani, ya kuwakilisha ufalme wa Mungu, alipewa mwanadamu. Lakini mwanadamu alidanganywa na kumuasi Mungu, nafasi ya Mungu ndani ya mtu, ilichukuliwa na shetani.

Mwanadamu anapomrudia Mungu, utukufu wa Mungu unateremka duniani katika ulimwengu wa roho. Hivyo utukufu wa Bwana ukitawala dunia, maskani ya Mungu inakuwa pamoja na wanadamu. Ufalme wa Mungu unapokaa duniani, ulimwengu wa roho uliopo Mbinguni na ule uliopo duniani, vinafanya kazi pamoja (Eze 37:27, Yoh 5:17, Efe 2:22, Luk 17:21). Mbinguni na duniani vinapofanya kazi pamoja, mwanadamu anapewa tabia ya Mungu, anafanya kile akitakacho Mungu kifanyike, anachukia kile akichukiacho Mungu. Katika injiri ya Yohana 5:19, anasema; “Mwana hawezi kutenda neno mwenyewe ila lile ambalo amwona Baba analitenda; kwa maana yote ayatendayo yeye, ndiyo ayatendayo Mwana vile vile. 20 Kwa kuwa Baba ampenda Mwana, naye humwonyesha yote ayatendayo mwenyewe; hata na kazi kubwa zaidi kuliko hizo atamwonyesha, ili ninyi mpate kustaajabu.21 Maana kama Baba awafufuavyo wafu na kuwahuisha, vivyo hivyo na Mwana awahuisha wale awatakao”.Pia unaweza kuona katika Maandiko yafuatayo;- Gal 2:20,1Yoh 5:4,1Yoh 3:6,3Yoh1:11,Yoh14:12, 15:4,1Yoh 2:27.
SABABU TANO(5) ZA MTU KUSHINDWA KATIKA MAJARIBU

Copy the BEST Traders and Make Money : http://ow.ly/KNICZ
SABABU TANO(5) ZA MTU KUSHINDWA KATIKA MAJARIBU

Copy the BEST Traders and Make Money : http://ow.ly/KNICZ
Kila mwanadamu kuna wakati hupitia katika majaribu ya aina mbalimbali katika maisha yake. Kuna majaribu ambayo huja kwa sababu ya kupungua kwa maombi, kuna majaribu yanayotokana na hila za watu, kuna majaribu yanayotokana tamaa ya mtu mwenyewe na pia kuna majaribu kama kipimo cha MUNGU kwa mtu wake ampendae. *Swali ni kwanini tunashindwa katika majaribu? zifuatazo ni sababu 5 za mtu kushindwa katika majaribu na hapa tunajifunza kwa kupitia mtumishi wa MUNGU Ayubu. SABABU 5 ZA MTU KUSHINDWA KATIKA JARIBU. 1:Wahudumu wetu katika majaribu. Ayubu 2:9.''Ndipo mkewe akamwambia, Je! Wewe hata sasa washikamana na utimilifu wako? Umkufuru Mungu, ukafe'' Hapa mke wa Ayubu ambaye alitakiwa awe ndiye anayemtia moyo mmewe yeye ndio kwanza alimwambia amkufuru MUNGU ili afe. Na hata leo wapo watu wengi sana ambao yawezekana uko kwenye jaribu fulani mfano ugonjwa lakini wao ndio kwanza ushauri wao kwako ni kwamba uende kwa mganga wa kienyeji ukawekewe jini ili upate nafuu kumbe ndio kabisa wanakupoteza. Hivyo wahudumu kwenye jaribu wanaweza kabisa wakasababisha ushindwe katika jaribu fulani hata kama ni dogo. 2:Marafiki tunaoshilikiana nao au wanaotutembelea wakati wa tatizo. Ayubu 2:12-13'' Basi walipovua macho yao, nao wakali mbali, wasimtambue, wakainua sauti zao na kulia; kila mmoja akararua joho yake, wakarusha mavumbi juu ya vichwa vyao kuelekea mbinguni. Kisha wakaketi nchi pamoja naye muda wa siku saba, mchana na usiku, wala hapana mmoja aliyenena naye neno lo lote; kwa maana waliona ya kuwa mashaka yake aliyo nayo ni makuu mno.'' Marafiki wakati mwingine wanaweza kuwa kikwazo cha mtu kushinda jaribu alilonalo na hapa tunajifunza kuhusu marafiki watatu wa ayubu ambao walikuja kumtembelea na badala ya wao kuwa faraja ndio kwanza walianza kumshutumu Ayubu kwamba haiwezekani awe hivyo lazima tu kuna dhambi amefanya na wanamwambia awaambie dhambi aliyofanya ili wamwombee kwa MUNGU na jaribu lake liishe kumbe wao ndio wakosaji na sio Ayubu.ndugu ni mara ngapi umepatwa na magumu na marafiki zako kuanza kukushutumu kwamba haiwezekani MUNGU ayaruhusu hayo kwako ni lazima tu umetenda dhambi kumbe hata dhambi hukutenda ila ni jaribu tu la kupima imani yako na baada ya kushinda jaribu hili unapandishwa kutoka utukufu hadi utukufu. Hivyo marafiki au watu wanaokutembelea wakati wa jaribu wanaweza kuwa sababu yako ya kushindwa kama ukiamua kuwasikiliza wakuambiacho. Hapa ayubu hakuwapa nafasi ndio maana alishinda majaribu hayo. Unaweza ukajiuliza kati ya Ayubu na wale rafiki zake ni nani alikua na mashaka? Marafiki zake walikua na mashaka kuliko hata mgonjwa mwenyewe na kama uko kwenye hali mbaya harafu wazima waliokuzunguka wao ndio wanalia hata wanashindwa kula hakika watazidisha ugonjwa kwako muhusika kamili. 3:Kujihesabia haki wakati wa majaribu. Ayubu 9:2''Kweli najua kuwa ndivyo hivyo; Lakini mtu huwaje mwenye haki mbele za Mungu?'' usijihesabie haki wakati wa jaribu na pia ndugu waliochini kiroho usiwasikilize sana wakati wa jaribu maana imani zao ni ndogo hivyo ni rahisi sana kukukatisha tamaa na kukupelekea uchukue maamuzi mabaya tena ukiwa karibu kabisa na ushindi wako. 4:Tusijilinganishe sana na wale ambao hawajaribiwi wakati huo. Ayubu 12:4''Mimi ni mtu wa kuchekwa na jirani yake, Ni mtu niliyemwita Mungu, naye akanijibu; Huyo mwenye haki, aliye mtimilifu, amekuwa ni kicheko'' Ndugu usikubali kujiringanishi na watu ambao hawajaribiwi wakati huo maana unaweza ukaanza kulalamika na kupelelea kukufuru kwa MUNGU na kuona kama unaonewa wewe tu huku wengine wakiishi kwa amani na furaha isipokua wewe tu. 5:Tusiwahusudu wasioamini. ukiwahusudu wasioamini utakuwa unajipoteza wewe mwenyewe pia ukiwahusudu wasioamni utakua unaanza kuikataa mbingu. HAYA YOTE HUPUNGUZA UWEZEKANO WA KUSHINDA MAJARIBU. MUNGU awabariki sana . Ni mimi ndugu yako Peter Michael Mabula.

Copy the BEST Traders and Make Money : http://ow.ly/KNICZ
Kila mwanadamu kuna wakati hupitia katika majaribu ya aina mbalimbali katika maisha yake. Kuna majaribu ambayo huja kwa sababu ya kupungua kwa maombi, kuna majaribu yanayotokana na hila za watu, kuna majaribu yanayotokana tamaa ya mtu mwenyewe na pia kuna majaribu kama kipimo cha MUNGU kwa mtu wake ampendae. *Swali ni kwanini tunashindwa katika majaribu? zifuatazo ni sababu 5 za mtu kushindwa katika majaribu na hapa tunajifunza kwa kupitia mtumishi wa MUNGU Ayubu. SABABU 5 ZA MTU KUSHINDWA KATIKA JARIBU. 1:Wahudumu wetu katika majaribu. Ayubu 2:9.''Ndipo mkewe akamwambia, Je! Wewe hata sasa washikamana na utimilifu wako? Umkufuru Mungu, ukafe'' Hapa mke wa Ayubu ambaye alitakiwa awe ndiye anayemtia moyo mmewe yeye ndio kwanza alimwambia amkufuru MUNGU ili afe. Na hata leo wapo watu wengi sana ambao yawezekana uko kwenye jaribu fulani mfano ugonjwa lakini wao ndio kwanza ushauri wao kwako ni kwamba uende kwa mganga wa kienyeji ukawekewe jini ili upate nafuu kumbe ndio kabisa wanakupoteza. Hivyo wahudumu kwenye jaribu wanaweza kabisa wakasababisha ushindwe katika jaribu fulani hata kama ni dogo. 2:Marafiki tunaoshilikiana nao au wanaotutembelea wakati wa tatizo. Ayubu 2:12-13'' Basi walipovua macho yao, nao wakali mbali, wasimtambue, wakainua sauti zao na kulia; kila mmoja akararua joho yake, wakarusha mavumbi juu ya vichwa vyao kuelekea mbinguni. Kisha wakaketi nchi pamoja naye muda wa siku saba, mchana na usiku, wala hapana mmoja aliyenena naye neno lo lote; kwa maana waliona ya kuwa mashaka yake aliyo nayo ni makuu mno.'' Marafiki wakati mwingine wanaweza kuwa kikwazo cha mtu kushinda jaribu alilonalo na hapa tunajifunza kuhusu marafiki watatu wa ayubu ambao walikuja kumtembelea na badala ya wao kuwa faraja ndio kwanza walianza kumshutumu Ayubu kwamba haiwezekani awe hivyo lazima tu kuna dhambi amefanya na wanamwambia awaambie dhambi aliyofanya ili wamwombee kwa MUNGU na jaribu lake liishe kumbe wao ndio wakosaji na sio Ayubu.ndugu ni mara ngapi umepatwa na magumu na marafiki zako kuanza kukushutumu kwamba haiwezekani MUNGU ayaruhusu hayo kwako ni lazima tu umetenda dhambi kumbe hata dhambi hukutenda ila ni jaribu tu la kupima imani yako na baada ya kushinda jaribu hili unapandishwa kutoka utukufu hadi utukufu. Hivyo marafiki au watu wanaokutembelea wakati wa jaribu wanaweza kuwa sababu yako ya kushindwa kama ukiamua kuwasikiliza wakuambiacho. Hapa ayubu hakuwapa nafasi ndio maana alishinda majaribu hayo. Unaweza ukajiuliza kati ya Ayubu na wale rafiki zake ni nani alikua na mashaka? Marafiki zake walikua na mashaka kuliko hata mgonjwa mwenyewe na kama uko kwenye hali mbaya harafu wazima waliokuzunguka wao ndio wanalia hata wanashindwa kula hakika watazidisha ugonjwa kwako muhusika kamili. 3:Kujihesabia haki wakati wa majaribu. Ayubu 9:2''Kweli najua kuwa ndivyo hivyo; Lakini mtu huwaje mwenye haki mbele za Mungu?'' usijihesabie haki wakati wa jaribu na pia ndugu waliochini kiroho usiwasikilize sana wakati wa jaribu maana imani zao ni ndogo hivyo ni rahisi sana kukukatisha tamaa na kukupelekea uchukue maamuzi mabaya tena ukiwa karibu kabisa na ushindi wako. 4:Tusijilinganishe sana na wale ambao hawajaribiwi wakati huo. Ayubu 12:4''Mimi ni mtu wa kuchekwa na jirani yake, Ni mtu niliyemwita Mungu, naye akanijibu; Huyo mwenye haki, aliye mtimilifu, amekuwa ni kicheko'' Ndugu usikubali kujiringanishi na watu ambao hawajaribiwi wakati huo maana unaweza ukaanza kulalamika na kupelelea kukufuru kwa MUNGU na kuona kama unaonewa wewe tu huku wengine wakiishi kwa amani na furaha isipokua wewe tu. 5:Tusiwahusudu wasioamini. ukiwahusudu wasioamini utakuwa unajipoteza wewe mwenyewe pia ukiwahusudu wasioamni utakua unaanza kuikataa mbingu. HAYA YOTE HUPUNGUZA UWEZEKANO WA KUSHINDA MAJARIBU. MUNGU awabariki sana . Ni mimi ndugu yako Peter Michael Mabula.

Copy the BEST Traders and Make Money : http://ow.ly/KNICZ
Kila mwanadamu kuna wakati hupitia katika majaribu ya aina mbalimbali katika maisha yake. Kuna majaribu ambayo huja kwa sababu ya kupungua kwa maombi, kuna majaribu yanayotokana na hila za watu, kuna majaribu yanayotokana tamaa ya mtu mwenyewe na pia kuna majaribu kama kipimo cha MUNGU kwa mtu wake ampendae. *Swali ni kwanini tunashindwa katika majaribu? zifuatazo ni sababu 5 za mtu kushindwa katika majaribu na hapa tunajifunza kwa kupitia mtumishi wa MUNGU Ayubu. SABABU 5 ZA MTU KUSHINDWA KATIKA JARIBU. 1:Wahudumu wetu katika majaribu. Ayubu 2:9.''Ndipo mkewe akamwambia, Je! Wewe hata sasa washikamana na utimilifu wako? Umkufuru Mungu, ukafe'' Hapa mke wa Ayubu ambaye alitakiwa awe ndiye anayemtia moyo mmewe yeye ndio kwanza alimwambia amkufuru MUNGU ili afe. Na hata leo wapo watu wengi sana ambao yawezekana uko kwenye jaribu fulani mfano ugonjwa lakini wao ndio kwanza ushauri wao kwako ni kwamba uende kwa mganga wa kienyeji ukawekewe jini ili upate nafuu kumbe ndio kabisa wanakupoteza. Hivyo wahudumu kwenye jaribu wanaweza kabisa wakasababisha ushindwe katika jaribu fulani hata kama ni dogo. 2:Marafiki tunaoshilikiana nao au wanaotutembelea wakati wa tatizo. Ayubu 2:12-13'' Basi walipovua macho yao, nao wakali mbali, wasimtambue, wakainua sauti zao na kulia; kila mmoja akararua joho yake, wakarusha mavumbi juu ya vichwa vyao kuelekea mbinguni. Kisha wakaketi nchi pamoja naye muda wa siku saba, mchana na usiku, wala hapana mmoja aliyenena naye neno lo lote; kwa maana waliona ya kuwa mashaka yake aliyo nayo ni makuu mno.'' Marafiki wakati mwingine wanaweza kuwa kikwazo cha mtu kushinda jaribu alilonalo na hapa tunajifunza kuhusu marafiki watatu wa ayubu ambao walikuja kumtembelea na badala ya wao kuwa faraja ndio kwanza walianza kumshutumu Ayubu kwamba haiwezekani awe hivyo lazima tu kuna dhambi amefanya na wanamwambia awaambie dhambi aliyofanya ili wamwombee kwa MUNGU na jaribu lake liishe kumbe wao ndio wakosaji na sio Ayubu.ndugu ni mara ngapi umepatwa na magumu na marafiki zako kuanza kukushutumu kwamba haiwezekani MUNGU ayaruhusu hayo kwako ni lazima tu umetenda dhambi kumbe hata dhambi hukutenda ila ni jaribu tu la kupima imani yako na baada ya kushinda jaribu hili unapandishwa kutoka utukufu hadi utukufu. Hivyo marafiki au watu wanaokutembelea wakati wa jaribu wanaweza kuwa sababu yako ya kushindwa kama ukiamua kuwasikiliza wakuambiacho. Hapa ayubu hakuwapa nafasi ndio maana alishinda majaribu hayo. Unaweza ukajiuliza kati ya Ayubu na wale rafiki zake ni nani alikua na mashaka? Marafiki zake walikua na mashaka kuliko hata mgonjwa mwenyewe na kama uko kwenye hali mbaya harafu wazima waliokuzunguka wao ndio wanalia hata wanashindwa kula hakika watazidisha ugonjwa kwako muhusika kamili. 3:Kujihesabia haki wakati wa majaribu. Ayubu 9:2''Kweli najua kuwa ndivyo hivyo; Lakini mtu huwaje mwenye haki mbele za Mungu?'' usijihesabie haki wakati wa jaribu na pia ndugu waliochini kiroho usiwasikilize sana wakati wa jaribu maana imani zao ni ndogo hivyo ni rahisi sana kukukatisha tamaa na kukupelekea uchukue maamuzi mabaya tena ukiwa karibu kabisa na ushindi wako. 4:Tusijilinganishe sana na wale ambao hawajaribiwi wakati huo. Ayubu 12:4''Mimi ni mtu wa kuchekwa na jirani yake, Ni mtu niliyemwita Mungu, naye akanijibu; Huyo mwenye haki, aliye mtimilifu, amekuwa ni kicheko'' Ndugu usikubali kujiringanishi na watu ambao hawajaribiwi wakati huo maana unaweza ukaanza kulalamika na kupelelea kukufuru kwa MUNGU na kuona kama unaonewa wewe tu huku wengine wakiishi kwa amani na furaha isipokua wewe tu. 5:Tusiwahusudu wasioamini. ukiwahusudu wasioamini utakuwa unajipoteza wewe mwenyewe pia ukiwahusudu wasioamni utakua unaanza kuikataa mbingu. HAYA YOTE HUPUNGUZA UWEZEKANO WA KUSHINDA MAJARIBU. MUNGU awabariki sana . Ni mimi ndugu yako Peter Michael Mabula.

Copy the BEST Traders and Make Money : http://ow.ly/KNICZ
SABABU TANO(5) ZA MTU KUSHINDWA KATIKA MAJARIBU

Copy the BEST Traders and Make Money : http://ow.ly/KNICZ
SABABU TANO(5) ZA MTU KUSHINDWA KATIKA MAJARIBU

Copy the BEST Traders and Make Money : http://ow.ly/KNICZ

Tuesday, 30 June 2015


Msamaha ni nini na kwanini ninauhitaji?


Neno “samehe” linamaanisha kusafisha nia au jambo nakulifanya kutokuwa na mawaa yoyote, ku achilia, kufutilia mbali deni. Tunapo kosea mtu, huuliza msamaha wao ili tukarudishe uhusiano. Msamaha haupeanwi kwa sababu mtu anastahili kusamehewa. Hakuna anaye stahili kusamehewa. Msamaha ni ishara ya upendo, huruma na neema. Msamaha ni uamuzi wa kutoshikilia jambo ndani yako kinyume cha mtu mwengine, haijalishi amekukosea kiasi gani.

Bibilia inatuambia yakwamba sote tunahitaji msamaha toka kwa Mungu. Sote tumefanya dhambi. Mhubiri 7:20 asema, “Bila shaka hakuna mwanadamu mwenye haki hapa duniani, ambaye afanya mema, asifanye dhambi.” 1Yohana 1:8 asema, “Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu.” Dhambi zote ni kitendo cha uasi kinyume chake Mungu (Zaburi 51:4). Basi kwa hivyo, tunahitaji kwa vyovyote msamaha wake Mungu. Kama dhambi zetu hazitasamehewa, tutakuwa katika adhabu ya milele tukiteseka kwa ajili ya madhara ya dhambi zetu (Mathayo 25:46;Yohana 3:36).

Msamaha-Je, ni upate vipi?

Kwa shukurani, Mungu ni mwenye upendo na huruma-mwenye ari ya kutusamehe dhambi zetu! 2Petro 3:9 asema, “Yeye hutuvumilia maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba.” Mungu anatamani kutusamehe, kwa hivyo alitoa kwa ajili ya msamaha wetu.

Adhabu ya haki pekee inayostahili kwa ajili ya dhambi zetu ni mauti. Sehemu ya kwanza ya kitabu cha Warumi 6:23 yasema, “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti…..” Mauti ya milele ndiyo ndiyo tuliyopokea kama mshahara wa dhambi zetu. Mungu, kwa mpango wake mahususi, alifanyika kuwa mwanadamu - Yesu Kristo (Yohana 1:1, 14). Yesu alikufa juu ya msalaba kwa kuchukua adhabu tuliyo stahili-mauti. 2Wakorintho 5:21 inatufundisha, “Yeye asiyejua dhambi alimfanya kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi tupate kuwa haki ya Mungu katika yeye. “Yesu alikufa msalabani, akichukua adhabu tuliyo stahili!Kama Mungu, kifo chake Yesu kilitoa msamaha wa dhambi kwa ulimwengu mzima. 1Yohana 2:2 asema, “Naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote. “Yesu alifufuka katika wafu, akishuhudia ushindi juu ya dhambi na mauti (1Wakorintho 15:1-28). Mungu apewe sifa kwa kupitia kifo na kufufuka kwake Yesu Kristo, Sehemu yote ya pili ya kitabu cha Warumi 6:23 ni kweli, “…bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.”

Je, ungetaka dhambi zako zisamehewe? Je, uko na hisia za kuudhi za kila mara zinazo kuhukumu na kuonekana kuwa ngumu ku epukika?Msamaha wa dhambi zako upo ikiwa utamwamini Yesu Kristo kama mwokozi wa maisha yako. Waefeso1:7 yasema, “katika yeye huyo, kwa damu yake, tunao ukombozi wetu, msamaha wa dhambi, sawasawa na wingi wa neema yake.” Yesu alitulipia deni ili tukapate kusamehewa. Unacho stahili ni kumuuliza Mungu akusamehe kupitia kwake Yesu, ukiamini yakwamba Yesu alikufa ili upate msamaha-naye atakusamehe! Yohana 3:16-17 ina habari hii ya ajab, “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye.”

Msamaha-Je, ni jambo lililo rahisi?

Ndio, ni rahisi! Huwezi kupata msamaha toka kwa Mungu. Huwezi kulipia msamaha wako toka kwa Mungu. Unaweza ku upokea tu, kwa imani, kupitia neema na huruma za Mungu. Kama unataka kumkubali Yesu Kristo kama mwokozi wako na kupokea msamaha toka kwa Mungu, hapa kuna ombi unalo weza kuomba. Kwa kusema ombi hili au ombi lengine lolote lile haiwezi kukuokoa. Ni kwa kumwamini Yesu Kristo pekee ndiko kutaleta msamaha wa dhambi. Ombi hili ni njia ya kumwelezea Mungu imani yako kwake na kwa kumshukuru kwa kukupea msamaha. “Mungu, najua ya kwamba nimefanya dhambi kinyume chako na ninastahili adhabu. Lakini Yesu Kristo akaichukua adhabu niliyo stahili ili kwa kumwamini yeye nipate kusamehewa. Ninaziacha dhambi zangu na nina weak imani yangu kwako ili niokolewe. Ahsante kwa neema yako kuu/ya ajabu na kwa msamaha! Amina.”

Je, umefanya uamuzi kwa Kristo kwa kile ulicho soma hapa? kama ndiyo, tafadhali bonyeza kwa “Nime mkubali Kristo hivi leo” hapo chini.

Saturday, 21 February 2015

SURA YA KUMI
NAMNA YA KUMSIFU NA KUMWABUDU MUNGU IPASAVYO

Moja ya sababu ya watu kutomsifu na kumwabudu Mungu ipasavyo, ni kutokujua namna ya kufanya sifa na kuabudu. Mambo/Pointi zifuatazo zitakusaidia kukuwezesha kujua namna ya kumsifu, kumwabudu na kumshukuru Mungu. Unapokuwa umetenga muda wa kusifu na kuabudu, au unapokuwa katika muda wako wa maombi, tumia ufahamu wako juu ya mambo uliyojifunza kuhusu Mungu, yanayomstahilisha kusfiwa na kuabudiwa. Kwa mfano:-

                                    A:                      MSIFU MUNGU KWA YALE MAMBO YANAYOMSTAHILISHA
1)      Mtukuze Mungu kwa Sifa zake za kipekee ( Sifa zake za Ki-Mungu).
Mweleze jinsi alivyo Mtakatifu, Wa milele, Mwenye nguvu zote, Mwenye akili na ufahamu wote, n.k

2)      Mtukuze Mungu kwa Tabia zake.
Mweleze jinsi alivyo mwenye Upendo mwingi usiopimika, jinsi alivyo na huruma nyingi, jinsi alivyo mwaminifu na wa kweli. Msimulie habari ulizozisikia na ulizozisoma juu ya tabia zake kwetu.

3)      Mtukuze Mungu kwa Matendo yake makuu.
Mweleze jinsi unavyohusudu kazi mbalimbali za mikono yake, uumbaji wake, na matendo yake makuu. Msimulie jinsi unavyokubali ubora wa kazi zake na ukuu wa matendo yake. Msimulie unavyothamini matendo yake makuu kutoka katika biblia au katika shuhuda ulizozisikia katika maisha ya sasa ya kila siku.

4)      Mtukuze Mungu kwa Baraka na Fadhili zake.
Msifu na kumshukuru kwa fadhili na baraka mbalimbali ulizopata kutoka kwake. Kwa zawadi ya uhai, afya njema, uponyaji, ulinzi, chakula, kazi, elimu, fedha, mali, mifugo, mashamba, biashara, n.k. Yako mambo mengi sana, Mungu amekutendea, usiyoweza kumaliza kuelezea. Msifu kwa hayo.
5)      Mtukuze Mungu kwa Ahadi zake nzuri kwetu.
Pia unaweza kumsifu Mungu kwa ahadi zake mbalimbali alizotupa. Ukampamba kwa jinsi alivyokusudia kutubariki, kutuinua, kutulinda, kutushindia, kututetea, kutuwezesha, kutusaidia, n.k.

                                    B:                    MSIFU MUNGU KWA MAJINA YAKE.
Majina ya Mungu, hueleza sifa za Mungu, Tabia za Mungu au Matendo ya Mungu. Mfano; Wayahudi wanamwita Mungu El-Shaddai. Ni neno lenye majina mawili ndani yake. El’  maana yake Mungu, na ‘Shaddai’ lenye maana itokanayo na neno ‘Shad’ yaani Titi (Ziwa) la mama anyonyeshaye.

Kutokana na ukweli kwamba, titi/ziwa la mama anyonyeshaye, linampa mtoto mchanga kila kitu anchohitaji. Maziwa ya mama yake, humpa mtoto kila kitu mtoto anachohitaji. Ndani ya maziwa kuna vitamini, protini, wanga, mafuta, madini, maji, na kila kitu mtoto anachohitaji. Maziwa ya mama, yanamtosheleza mtoto kwa kila kitu. Hivyo, Waisraeli wanapomwita Mungu El-Shaddai, wanamaanisha kuwa, kama ziwa linavyo mtosheleza mtoto, vivyo hivyo, Mungu ni ‘Mtoshelezi’ kwetu. Halleluyah!

Hivyo, kila jina la Mungu, linabeba aidha Sifa yake au Tabia yake au Matendo yake. Ndio maana Mfalme Daudi anasema “… Mpeni Bwana, enyi wana wa Mungu … Mpeni Bwana utukufu kwa jina lake. Mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu.” (Zab 29:1-2) Msifuni Bwana kwakuwa Bwana ni mwema, Liimbieni Jina lake, kwakuwa lapendeza.(Zab 135:3). Unaweza kumsifu Bwana kwa majina yake. Yafuatayo ni baadhi ya majina ya Mungu kwa lugha ya Kiebrania, yatakayokusaidia kumsifu, kumwabudu na kumshukuru Mungu.


Wednesday, 31 December 2014

UTAKATIFU
Mama Teresa wa Calcutta alichagua njia ya utakatifu Katika Biblia Yako Soma

1Pet 1:3-25; Zab 15

Mstari wa Kukariri
“Ee Mungu, uniumbie moyo safi, uifanye upya roho iliyotulia ndani yangu. Usinitenge na uso wako, wala roho wako mtakatifu usiniondolee. Unirudishie furaha ya wokovu wako; unitegemeze kwa roho ya wepesi (Zab 51:10-12).
Baadaye Zungumzieni Jambo Hili
Je, Ni Wapi Unapohisi Kwamba Sheria Ulizojiwekea Mwenyewe Au Ulizowekewa Na Watu Wengnie Zinagusa Maisha Yako?
Jambo La Kufanya Kabla Hatujakutana Tena 
Uwe mtakatifu kama Mungu alivyo mtakatifu kwa kufanya yale ayafanyayo Mwenyewe, kuwapenda wengine na kuishi kwa ajili yao. Uwe mtakatifu na kwa uhuru kabisa wafanyie watu jambo jema hata wale wasiostahili.
Kazi Ya Kuandika Ya Stashahada
Fanya uchambuzi wa masuala ya sheria na neema. Andika ukurasa mmoja kuhusu sheria unazoweza kuzipata na misimamo mbadala katika neema.
Tafakari Andiko Hili Neno Kwa Neno
2Kor 6:17 – 7:1
Tumia Dakika Moja Kuubadilisha Ulimwengu
Omba kwa ajili ya Wapalestina. Idadi yao ni karibu 2,000,000. Ni Waarabu Waislamu.

1. Je, Utakatifu Ni Nini?
Jibu lake ni rahisi, neno utakatifu lina maana ya kutengwa kwa ajili ya Mungu Baba, na kumwishia Yeye kwa namna inayompendeza. Utakatifu unaonekana katika maisha ya Yesu, na katika maisha ya mkristo anayekua kiroho. Ni mfumo wa maisha ambao Mungu anautaka kwa watu wake anaowaita watakatifu.
2. Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, Bwana Mungu Mwenye Uweza
Je ulijua kwamba Mungu si mtakatifu mara moja tu, lakini kwa sababu ya nafsi tatu zinazofanya Mmoja, yeye ni mtakatifu mara tatu? Ndivyo anavyosifiwa mbinguni na duniani (Isa 6:3) (Ufu 4:8).
Yesu alisema,”Baba Mtakatifu” (Yn 17:11).
Yesu ni Mtakatifu na Mwenye Haki (Mdo 3:14).
Roho wa Mungu ni Roho wa utakatifu (Rum 1:4).
3. Mwe Watakatifu, Kwa Kuwa Mimi Ni Mtakatifu
Watoto wafanane na Baba yao; huo ndio mwito wa Mungu kwa kila mmoja katika familia yake. Yafaa watu wamfahamu Baba yetu kwa kututazama sisi (1Pet 1:15, 16). Sisi ~
Tumechaguliwa kuwa watakatifu (Efe 1:4).
Tumeitwa kuwa wanaume na wanawake watakatifu (1The 4:7).
Tumeitwa kuwa kanisa takatifu (1Kor 1:2).
Tumepewa neema ya kuwa watakatifu (2Tim 1:9).
4. Aina Mbili Za Utakatifu
Kwanza kabisa, kuna kazi ambayo Kristo mwenyewe aliikamilisha pale Msalabani ya kutusamehe dhambi zetu na kututakasa; hiyo peke yake inatufanya watakatifu na kukubalika mbele za Mungu. Utakatifu huu hautokani na lo lote tunalofanya au tusilofanya. Sisi tumefanywa watakatifu kwa sababu katika neema yake Yesu alitwaa kutoka kwetu hali ya kukosa utakatifu na badala yake akatupatia utakatifu wake mwenyewe, la sivyo tusingeweza kamwe kuingia kwenye uwepo wa Mungu (Ebr 2:11; 13:12; 10:10).
Ni Mwanzo Tu, Bado Hatujakamilika
Lakini ingawa tumefanywa watakatifu mbele za Mungu, katika uzima na kuishi bado tunaendelea kufanywa watakatifu. Mapambano dhidi ya dhambi, ubinafsi na Shetani, na safari ya kuelekea kwenye ukamilifu wa maisha matakatifu Kutakuwa na kuanguka kwingi na kushindwa kwingi njiani (Ebr 10:14).
5. Tunataka Kuwa Watakatifu, Lakini Kwa Namna Gani?
Je, hili ni suala la mtu kuamua kuwaza mawazo mazuri zaidi, kusema maneno ya upole zaidi na kufanya mambo mema zaidi mara kwa mara? Maamuzi yote ya jinsi hiyo hayafai kitu kama watu wengi wanavyofahamu.
Mapambano Kati Ya Kujihesabia Haki Na Neema
Kutokana na hali ya kutaka kuwa safi na watakatifu, vizazi vya waamini wamefikia hatua ya kujihesabia haki kuhusiana na namna wakristo wanavyopaswa kuishi, wakibeba na kuwatwisha wengine mizigo ya sheria. Sheria zenyewe wakazivunja, na hivyo kushindwa.
Sheria
Mwamini anayejihesabia haki hutafakari kuhusu ni lipi afanye au ni lipi asifanye kwa kujiuliza mwenyewe iwapo mambo kama dansi, mvinyo, fedha, fasheni, sinema, na mitindo ya nywele ni uovu au hayana maana kwa wakristo. Anafanya maamuzi, anajidhibiti mwenyewe na kuwahamasisha wengine kuifuata sheria yake mpya. Matokeo yake wakristo wengi mara kadhaa wameshindwa kuwa chumvi na nuru katika shughuli mbalimbali za hadhara, na hivyo kuwafanya wasioamini bado kujichagulia mwelekeo wao wenyewe.
Neema
Neema inasema kwamba hakuna hata moja katika hayo lililo ovu au ambalo halina maana kwa wakristo; la msingi hapa ni namna tunavyoamua kutumia vitu hivyo. Kwa mfano, neema inasema kwamba uovu uko kwenye matumizi ya pombe na sio pombe yenyewe. Uovu uko katika kupenda fedha na sio fedha zenyewe. Hakuna uovu katika kucheza dansi ila katika sababu za kucheza.
Tusonge mbele Na Roho Mtakatifu
Iwapo utaamua kuchagua sheria au neema kuwa mtindo wa maisha yako, lakini ujue kwamba utakatifu wa kweli unapatikana kwa Roho Mtakatifu pekee ambaye asili yake ni utakatifu kama jina lake mwenyewe lilivyo – Mtakatifu.
Kujazwa kila siku na Roho Mtakatifu maana yake ni kwamba mwili, nafsi, na roho ya mwamini wakati wote anaendelea kuwa amefurika kwa kujawa na huyo mtu mtakatifu; akiendelea kuchuja kila wazo, neno na tendo la huyo mwamini , na kuwa mvumilivu katika kumletea maisha matakatifu kwa ndani, maisha yanayokubaliana na kila neno la Mungu, lakini yasiyotegemea juhudi za kibinadamu. Mara atafanya uwepo wake kujulikana, na unapofanya kosa au kutamka neno ovu, anashuhudia ndani ya moyo wako.
6. Njia Ya Utakatifu
Matakwa yetu na maamuzi yetu ni muhimu katika njia ya utakatifu. Kazi ya Maandiko ni kutuelekeza. Hapa kuna changamoto moja kutoka katika Kum 22:9-11:
Usipande aina mbili za mbegu katika shamba lako la mizabibu; ukipanda, utakuwa umetia unajisi mazao uliyopanda pamoja na matunda yake.
Usilime shamba kwa kuwafunga pamoja ng’ombe na punda kwenye kongwa moja.
Usivae nguo yenye mchanganyiko wa sufu na pamba.
Kataa Mchanganyiko Wa Mbegu Usio Mtakatifu
Mbegu zinapopandwa na kumwagiliwa hutoa mazao yanayofanana nazo. Kwahiyo panda mbegu moja tu ya neno la Mungu, yaani kweli; na kamwe usichanganye kweli ya Mungu na hekima ya ulimwengu huu, la sivyo utavuna zao la kuchanganyikiwa.
Kataa Mchanganyiko Wa Ushirika Usio Mtakatifu
Ni watu wawili pekee wanaompenda Mungu na wanaoamini Maandiko wanaoweza kuwa mmoja katika ndoa, au wamoja katika biashara. Soma yale aliyoyasema Paulo kwa habari ya kufungiwa nira katika 2Kor 6:14-17.
Kataa Mchanganyiko Wa Mavazi Usio Mtakatifu
Uvaaji aliotupa Mungu ni vazi la haki na kufunikwa na uweza utokao juu. Ikiwa leo tutavaa mavazi ya Mungu na kesho tukavaa mavazi ya ulimwengu, kamwe hatutakuwa watakatifu, na wala hatutafanana na jinsi ambavyo Baba anataka sisi tuwe (Isa 61:10) (lk 24:49). Njoo Ee Roho Mtakatifu utujaze na kutusaidia.