Friday, 3 May 2013

Soma kwa Kumbukumbu Zako Maneno haya Ya Lowassa.

"Mheshimiwa Spika, kwanza napenda kuchukua nafasi hii kukushukuru sana kwa kunifanya msemaji wa kwanza katika hoja hii.
Lakini la pili, nimpongeze Dk. Harrison Mwakyembe, Mwenyekiti wa Kamati Teule kwa kuwasilisha kwa mbwembwe nyingi sana taarifa yake, mbwembwe zilikuwa nzuri kweli.

Kwa kazi nzuri kwa maoni yao, wamewasilisha vizuri. Lakini nimesimama kuweka kwenye kumbukumbu kutoridhika kwangu na jinsi kazi hiyo ilivyofanywa.

Mheshimiwa Dk. Harrison Mwakyembe ni mwanasheria, alikuwa anafundisha wanafunzi Chuo Kikuu. Moja ya vitu alivyokuwa anafundisha ni 'NATURAL JUSTICE'.

Mheshimiwa Spika, wewe pia ni mwanasheria unafahamu suala la 'NATURAL JUSTICE'. Kwamba Kamati Teule imesikiliza watu wengine wote pamoja na wanaoita minong'ono ya mitaani. Wamesafiri mpaka Marekani kutafuta mashahidi, lakini mimi ambaye ni mmoja katika watuhumiwa mle hawakunihoji hata siku moja.

Mheshimiwa Spika, nimesimama kueleza masikitiko yangu. Ofisi ya Bunge mpaka ofisini kwangu (Dar es Salaam) hata wangeniita ningekwenda kwa miguu kama hamna gari na nilikuwa tayari kufanya hivyo.

Hawa ni watu makini sana siwezi kuamini kwamba wanaweza wakafanya 'oversight' kama hiyo. Kwa sababu katika kila hoja walizojenga wamesema 'Waziri Mkuu ilikuwa hivi'. Kulikuwa na shida gani kuja kuniuliza 'Waziri Mkuu wanasema ulitoa dokezo hili ni sawa sawa ni kweli'? Kulikuwa na shida gani kwa mfano kufuata utaratibu wa Westmister kuthibitisha hapo unaposema mwenye Richmond ni fulani uka-lay on the table records na ushahidi kuwa ni fulani.

Mheshimiwa Spika, Taifa letu ni Taifa changa, lakini chombo hiki ndiyo mahali pa demokrasia pakubwa katika nchi pote, hapa ndipo penyewe.

Kama katika chombo hiki hakitaonekana kutendeka haki nchi yetu haitakwenda vizuri. Hapa ndipo tunategemea tuwaonyeshe umakini wetu, umahiri wetu katika mambo ya demokrasia.

Kwa hiyo, nilichofanyiwa napenda kuweka kumbukumbu sawa kwamba, naona si sahihi, NIMEFADHAIKA SANA, NIMEDHALILISHWA SANA, NIMEONEWA SANA KATIKA HILI.

Maana zimechukuliwa tuhuma zikaja zikaelezwa hapa kwamba hivi ndivyo ilivyo. Mimi sijaulizwa. Kulikuwa na shida gani ya kuniuliza, kwa nini muamini minong'ono ya mitaani kuliko maelezo zangu?

SISI WOTE HAPA NI WANASIASA, TUKIANZA KUAMINI MINONG'ONO YA MITAANI NIAMBIENI MWANASIASA ATAKAYESIMAMA. Hatuwezi, Tume imepewa muda wa kutosha lakini inashindwa kumuona mtu ambaye wanamtuhumu na wanamsema kwa kirefu sana.

Mheshimiwa Spika, lakini hata pale uliponinong'oneza ukaniambia una ushahidi wowote? Nilikuwa na ushahidi huo wa maandishi.

Katika taarifa yao hakuna hata moja ya ushahidi ambao umetoka kwa Waziri Mkuu. Kile kitabu cha majedwali kimejaa majedwali mengi pamoja na magazeti mpaka ya udaku lakini maelezo ya Waziri Mkuu hakuna hata moja.

Mheshimiwa Spika naamini ingekuwa ni heshima kubwa wangeiweka halafu wakasema tunakataa kitambulisho hiki kwa sababu hii na hii, hiyo ndiyo imejengwa hoja.

Lakini kujenga hoja na kuja hapa bungeni tunahutubia nchi nzima na kusema Waziri Mkuu amefanya hiki, amefanya hiki bila ya kumsikiliza nachelea kuuliza hivi mtu wa chini itakuwaje?

Mheshimiwa Spika, lakini nimetafakari kwa makini sana jambo hili nikajiuliza hivi hasa kulikoni mpaka watu wazima, wenye uwezo wao, watu maarufu wenye heshima zao, mpaka wafike mahali waache jambo la msingi kama hilo, kulikoni?

Mimi nadhani there is a wish which I am going to grant, ni Uwaziri Mkuu. Kwamba ionekane Waziri Mkuu ndio amefanya haya, tumuondolee heshima au tumwajibishe.

Mheshimiwa Spika, nimetafakari sana kwa NIABA YA CHAMA CHANGU, KWA NIABA YA SERIKALI YANGU nimeamua kumwandikia Rais barua ya kumwomba niachie ngazi.

Nafanya hivyo kwa moyo mweupe kabisa ili kuonyesha DHANA YA UWAJIBIKAJI lakini na KUTOKUBALIANA NA UTARATIBU ULIOTUMIKA KUSEMA UONGO NDANI YA BUNGE WA KUMSINGIZIA MTU.

Edward Lowassa (MP),
Rtd PM..

Think Twice..
3Like · ·
  • 35 people like this.
  • Faith Therichgal Pelle Reading his made me hear his voice, got emotional and I think utabiri wake unatimia somehow....mtu kama huyu aliyesalitiwa itakua vema tukimpa uraisi maana utayafichua mengi hopefully.
  • Meigaro Olle Moikan Mimi natoka jimbo la EL. Kimsingi simfagilii huyu Mheshimiwa, lakini kuna mambo mengi ambayo kwa kweli nakubaliana naye kuliko mtu mwingine yeyote huko CCM. Hili lilipotokea wala sikuona kama shida iko kwake bali kwa chama anachokitumikia. Nilitamani sana aondoke CCM ...!
  • Mujuni Mutembei Hii ilikuwa hotuba ya kugusa sana wakati ule na hata sasa. Na yawezekana ni kweli hakuwa na hatia. Lakini mh. Lowassa alikuwa na nafasi ya kukataa tuhuma zilizotolewa juu yake na nikikumbuka na yale aliyoyasema katika kikao cha ccm mwaka jana kule dodoma, alikuwa na ushahidi wa kumtakatisha na kuelezea ukweli kwa umma wa watanzania kuhusu kile kilicho kuwa na mushkeri hasa. Pia aliwajua watu waliohusika katika sakata zima la richmond. Tume ya akina mwakyembe ilishindwa kupin out muhusika hasa na hivyo kuamua kumtega yeye maana walijua kama ni muungwana angesema aliyehusika hasa. Bahati mbaya kwa usalama wa taifa, serikali na chama tawala Lowassa aliamua kujitoa mhanga.

    Kwa upande mmoja hili laweza kuwa jambo la kishujaa lakini kwa upande mwingine hili ni jambo la woga.

    Huyu ni potential leader lakini sera na msimamo wa waliomzunguka uliharibu wasifu wake.

    He was drinking with the wrong guys
  • Meigaro Olle Moikan Mwakyembe alisema mambo mengine yamefichwa kwa sababu za Usalama wa Taifa! Hili kwangu lilikuwa linamaanisha kuwa hata Rais JK anaweza kuwa anahusika. Ndiyo maana wakaficha ficha majibu ya maswali mengine magumu na kumtoa kafara EL, ambaye kwa wakati huo alionekana kumfunika sana rafiki yake kwa utendaji na upeo!
  • Richard Zuberi Mwombeki ushahidi lazima atakuwa anao ndio maana analalamika hawajamhoji wakati ofisi yake ipo karibu na ofisi ya bunge. Sio kusahau au kusamehe, kwani kipya kipi alichokifanya yeye mbona watu wengi wanatajwa katika kashfa lakini hawajajiuzulu.
  • Martha Lucass Mh.Lowasa amewahi kusema alikuwa akisaini mikataba kwa kumsikiliza Rais ss iweje kweny ufisadi awe mwenyewe wkt maamuzi alikuwa akishirikisha baadhi ya watu ndo anafanya? So jibu unalo ww Mtz.
  • Mwombeki Fabian Richard Zuberi Kwan kujiuzulu ndo evidence ya kutohusika? Kwann hakujitetea?
  • Mujuni Mutembei True kwanini hakujitetea
  • Richard Zuberi Mimi sina uhakika kama amehusika au la, but kujiuzulu kwangu mimi ni evidence ya kiongozi aliye kiongozi kweli. Mwombeki watu wamekufa kwa kupigwa na mabomu kutoka ktk maghala ya jeshi lakini hakuna aliye tayari kujiuzulu, wanafunzi wanafeli kupitiliza lakini hakuna wa kujiuzulu.
  • Mwombeki Fabian Richard Zuberi Kwan swala ni kujiuzulu au kuhusika? Kujiuzulu ni kuwahubika kwamba hukuwa makin kiuongozi na hatuwezi kukuamin tena kimaamuzi. Richmond na mbagala tofauti. Hata kama wote wangejiuzulu bado tungewawajibisha tena.
    Tatizo hapa naona ni il
    ...See More
  • Mujuni Mutembei Hatukufundishwa kukimbia majukumu bali kuyakabili
  • Mujuni Mutembei Lowassa alikimbia.
  • Richard Zuberi Hawakumpa plaform ya kujitetea, na kwa ilipofika kama wao wana tume wanasema kuna mambo hawakuyasema kwa sababu za kiusalama may be, so inawezekana hata yeye kwa level ya tatizo lilipofika angejitetea labda angeibua matatizo zaidi so kwa hekima aliona bora astep down. He is one of the great leaders of our nation.
  • Richard Zuberi Mwombeki we una uhakika alihusika, au alikuwa akitenda sawa sawa na maelekezo ya mkuu wake wa kazi?
  • Mwombeki Fabian Great leader? Really? Share his track record as a leader. He has immense wealth mostly accrued during his public office tenures.
    We don't know his business dealings but he is known to have phantoms of financials allover the country.
    To me, any politician who becomes rich during his political career is questionable. Most likely an embezzler of public funds.
  • Richard Zuberi So you want politicians to be poor? I better choose a rich politician as long as he does something than a poor one who does nothing.
  • Richard Zuberi Ni bora niwe na muuza duka langu anayeiba elfu hamsini halafu ananiletea faida ya laki tano kwa mwezi kuliko ambaye haibi hata shilingi lakini ananiletea hasara kila siku. I will always uphold Lowasa as a great leader kama ni weaknesses kila kiongozi wa kiafrika anazo.
  • Mwombeki Fabian How can a politician in office become richer than a businessman in Kariakoo just by being in power? From what sources? Rich people can be politicians but poor politicians can't be rich just by becoming politicians. We all know their remunerations as pu...See More
  • Godfrey Kamwaya duniani hakuna mtu mbaya kwa kila jambo....alikuwa na yake mazuri.....baniani mbaya kiatu chake dawa......
  • Himson Exaud Naona kama hapa kambwela mbwela tu, i still can't see any evidence of innocence....! His guilty is within the spectrum of possibility unless justfied...!
  • Mujuni Mutembei Issue sio kuwa rich au poor. Issue ni kipi alisema ambacho hakimuincrimanate. Hatuna uhakika kuwa hakuhusika lakini pia hatuna uhakika kama alihusika. Platform alipewa tena bungeni lakini hakuitumia. Aliulizwa lakini hakujibu. Mimi nasema alificha jambo. Na jambo hilo alilolificha ndo lililomuangamiza.
  • Mujuni Mutembei Kweli exaud. Hakutaka kujustify kwanini anasema wanamuonea.
  • Oscar R. Nyirenda Kama alihusika au la anajua vizuri yeye na Mungu. Katika uongozi ni kweli kuna level ukifika huwezi sema kama ambavyo wengine tungefikir kusema. Wengi hapa tunalinganisha na uongozi wa vyuoni au makundi mengine ambayo labda mwenyekiti kumtaja katibu au...See More
  • Richard Zuberi Ukiwa politiciana haujafungwa mikono kuwa businessman. Mtu mwenye busara anajua sio tu aongee nini lakini pia aongee wapi na wakati gani. He is a great leader.
  • Oscar R. Nyirenda Unless tume assess na kujiridhisha kuwa mali zake kaiba, otherwise mimi sioni kosa maana haikuwa nchi ya kijamaa tena.
    Ninachojua na kuamini ni kuwa ukiwa ktk system yoyote unapata fursa kuliko aliyenje. Si hata waalimu wanauza visheti?? Wanasheria wa serikali wanafungua law firms??, madactari si ndio wenye maduka ya dawa??, makampuni ya ulinzi nayo ni ya kina nani??
  • Himson Exaud @Richard Zuberi, on your view and ur political attitude you may be right but you are critically wrong by facts....ha
  • Mwombeki Fabian Oscar R. Nyirenda na mwanasiasa anafanya nn?
  • Oscar R. Nyirenda Haa haa haa Dr. Mwombeki Fabian mwanasiasa akiona fursa ya mradi mkubwa wa MES wa miaka miwili ijayo ataanzisha kampuni kubwa ya wakala wa kuuza saruji bati nondo n.k hata kama sio kwa jina lake.
    Akiona fursa ya kusambaza mahindi ya msaada mikoani na
    ...See More
  • Richard Zuberi Mwombeki zaidi ya kuuliza maswali una nini cha ziada cha kusema?
  • Mwombeki Fabian Richard Zuberi i have said enough hapo juu. Lowasa had his chance to clear his name but he decided to chick-out and leave. His office was incriminated by the parliament's report. I can only accuse him by the evidence stipulated in that report but i can...See More
  • Mujuni Mutembei Lakini tunatetea nini
  • Mujuni Mutembei Kama ni msafi na aseme basi
  • Richard Zuberi Kutuhumiwa haina maana una makosa na si lazima ujitetee, ndio maana aliposimama bungeni alisema, there is a wish to be granted, alijua watu wanataka kutumia ushahidi wa mitaani kumtoa ktk uwaziri mkuu, aliona awape wanachotaka, hata Yesu alihukumiwa bi...See More
  • Mwombeki Fabian Richard Zuberi kukaa nje? Wakati hii linatokea I was around. Anyway lets agree to disagree. I was just airing my views and not trying to convince you.
  • Nsia Janeth Mwasha kaka osca me nafikiri tufike mahali tuwe wawazi,kama aliona kuna jambo halifahamiki angezungumza ili ajiokoe yeye lakini pia aliokoe taifa kwasababu tatizo lilishawekwa wazi kitaifa na lilikua likitatuliwa hvyohvyo likiwa naked yeye hakuwa na haja ya kuanza kulistili.kwangu mimi hyo ni kuficha maradhi...
  • Mujuni Mutembei Hii sio sahihi. Unasema Yesu hakujitetea, He answered all the qns on him. Waliposema eti wewe ni mfalma alisema wewe wasema.
  • Samuel Sasali Ni vile tu Report ilisomwa Bungeni lakini Kuna Report ya Hela Za Uswisi akina Chenge Bilioni 1 na ushahidi akiwa Mwanasheria Wa Serikali, Mpaka sasa tuna Utata wa Issue ya Kifo Cha Mhe. Balali, EPA ile pale. Mimi nakubali Kabisa Lowassa ana Mijihela ya...See More
  • Mwombeki Fabian Samuel Sasali swali ni je hakuhusika ? Alionewa? Alibambikiziwa? Hakuwa na jinsi ya kusema ukweli kwa niaba ya wananchi?
  • Mujuni Mutembei Yote hayo tisa lakini hayamsafishi lowassa. Wa kumsafisha lowassa ni yeye mwenyewe lowassa. Inabidi a-man up. Aseme ukweli. Asikubali kuficha maovu ya wengine. Huwezi kuficha ukweli eti kwa maslahi ya taifa. Nilitangulia kusema mwaka jana kwenye kikao cha ccm alijaribu kuongea ambayo angeyaongea 2008 bungeni
  • Richard Zuberi Mwombeki the only thing you have are questions nothing else.
  • Richard Zuberi Yeah Mwombeki lets agree to disagree.
  • Samuel Sasali Alishiriki sababu ali approve....ALISHIRIKI..
  • Samuel Sasali Mujuni Mutembei nakubaliana na wewe kabisa alichoongea mwaka jana ndicho alipaswa kuongea Bungeni siku Ile, mimi sijui kwanini anaogopa kusema Ukweli...
  • Mwombeki Fabian Richard Zuberi you need to read the whole thread. You are accusing me of improprieties that are neither true or clear. Yes, I have qns but I also state my views. Whats yours?

    Your sentiments are indeed supportive of mheshimiwa but you don't offer cr
    ...See More
  • Richard Zuberi I thought we had already agreed to disagree @Mwombeki.
  • Mwombeki Fabian Richard Zuberi just a closing argument to your last but one comment.
    Ok 'Roma locuta; causa finita est'
  • Samuel Sasali hahaha kwa vile tu Mabwe Pande iko Tanzania lakini Ukweli tukizingatia hawa waliopo The Guy is Great.....
  • Richard Zuberi Hahahahah! I better have a live dog than a dead lion.