Friday, 31 May 2013

ILIWEZEKANAJE YONA KUKAA TUMBONI MWA SAMAKI KWA SIKU TATU?

Yawezekana kabisa ukawa una maswali mengi juu ya uwezekano kwamba Yona yule aliyetumwa kuhubiri Ninawi aliweza wezaje kukaa ndani ya tumbo la samaki pasipo kumeng’enywa kama vyakula vingine kwa siku tatu? Wanasayansi wanajaribu kufafanua namna ambavyo jambo hilo linawezekana na hivyo kuthibitisha kwamba Mungu wetu yu hai na anaweza kufanya mambo makubwa na ya ajabu.

Ukiaacha ya Yona zipo hadithi nyingi za watu waliomezwa na nyangumi na kisha kutoka wakiwa hai. Hizi sio hadithi za yule nondo mla watu wa ziwa Jipe bali ni kweli. Samaki mkubwa aitwaye "Sea Dog" (Carcharodon carcharias), anayepatikana kwenye maji ya bahari yenye mkondo joto huweza fikia urefu wa futi 40. Kunako miaka ya 1758 mvuvi mmoja bahari ya Mediterania aliwahi kuangukia baharini na kumezwa na samaki wa aina hii. Nahodha wa meli hiyo aliamuru bomu lipigwe kumlenga yule samaki. Matokeo yake ni kwamba yule samaki alimtapika mvuvi akiwa hai pasipo madhara yeyote. Maka 1891, James Bartley- mvuvi mwingine nae alimezwa na nyangumi katika visiwa vya Falkland na alikaa ndani ya nyangumi huyo kwa zaidi ya masaa 48 mpaka samaki huyo alipovuliwa na kupasuliwa. Ilimchukua wiki mbili kuweza kurejea katika hali yake ya kawaida lakini alipona. Wako watu wengi tu ambao wanatajwa kumezwa na kisha kutapikwa na nyangumi wakiwa hai.

Wataalamu wa mambo ya kale wanaandika kwamba Babeli ilikuwa na utamaduni wa kuamini Samaki Mtu (Nguva). Wanasema kunako mwanzoni mwa ustaarabu (civilization) Ukaldayo na Babeli uliamini sana maongozi ya mtu ambaye alikuwa nusu mtu nusu samaki aliyetoka majini. Katika siku za Yona, Ninawi nayo pia ilikuwa katika mfumo huo wa kiimani na waliamini katika roho iliyoleta ujumbe kupitia mtu aliyetokea/kuibuka kutoka majini/baharini kama nusu mtu, nusu samaki. Kwa maana hiyo basi hatushangai kuona hata ujumbe wa Yona ulipata kukubaliwa kwa haraka sana na watu wa Ninawi hata kutubu na kuziacha dhambi zao, na pia twasoma katika biblia kwamba Mungu aliusamehe mji wa Ninawi.

Tunaposoma leo katika biblia juu ya habari za Ninawi ni kama hadithi lakini ni mji uliokuwapo na wanasayani wanathibisha masalia yake kama yalivyochimbuliwa huko Babeli yajulikanayo kama "Neby Yunas," . Katika masalia hayo kuna kumbukumbu za jina la YONA (Yunas) jambo linalothibitisha hadithi hiyo ya Yona na pia waliweza kugundua masalia yaliyoharibika ya kasri ya mfalme wa Ninawi.

Kwa nini tuombe? Kuna haja gani ya kuomba wakati Mungu anajua kesho na bado ni yeye anatawala. Ikiwa hatutaweza badilisha mawazo ya Mungu kwa nini tuombe?

Swali: "Kwa nini tuombe? Kuna haja gani ya kuomba wakati Mungu anajua kesho na bado ni yeye anatawala. Ikiwa hatutaweza badilisha mawazo ya Mungu kwa nini tuombe?"
Jibu: Kwa Mkristo, maombi ni kama kupumua. Ni rahisi kufanya kuliko kutofanya. Tunaomba kwa ajili ya sababu mbalimbali. Kwa sababu moja maombi ni njia ya kumtumikia Mungu (Luka 2:36-38) na kumtii. Tunaomba kwa sababu Mungu anatuamuru kuomba (Wafilipi 4:6-7). Maombi yamedhihirishwa kwetu na Yesu pamoja na kanisa la kwanza (Mariko 1:35; Matendo Ya Mitume 1: 14; 3:1; 4: 23-31; 6:4; 13:1-3). Kama Yesu aliehesabu kuwa maombi ni kitu cha maana, pia nasi lazima. Kama aliitajika kuomba ili asalie katika mapenzi ya Baba yake, je tunahitajika kuomba kiazi gani?

Sababu nyingine ya kuomba ni kuwa Mungu anataka maombi yawe njia kupata suluhisho lake kwa hali zetu. Tunaomba tukijiandaa kufanya maamuzi muimu (Luka 6:12-13); ilitushinde vizuizi vya shetani (Mathayo 17:14-21); kukusanya wafanyi kazi kwa sababu ya mavuno ya kiroho (Luka 10: 2); kupata nguvu ili tuyashinde majaribu (Mathayo 26:41); na kupata njia ya kuwatia wengine nguvu kiroho (Waefeso 6:18-19).

Tunakuja kwa Mungu katika mahitaji yetu kamili, na tuko na ahadi ya Mungu kwamba maombi yetu si ya bure, hata kama hatupati chenye tunauliza (Mathayo 6:6; Warumi 8:26-27). Ameahidi kuwa tunapouliza vitu ambavyo viko katika mapenzi yake, atatupa chochote tuitizacho (1 Yohana 5: 14-15). Wakati mwingine anakawisha majibu yake kulingana na hekima yake kwa manufaa yetu. Katika hali hii tunastahili kuwa makini na kudumu katika maombi (Mathayo 7:7; Luka 18:1-8). Maombi yasionekane kama njia zetu za kumfanya Mungu kutenda mapenzi yetu duniani, bali iwe ni njia ya Mungu kutenda mapenzi yake duniani. Hekima ya Mungu inapita hekima yetu.

Kwa hali ambazo hatuwezi jua mapenzi ya Mungu kamili, maombi ni njia ya kutambua mapenzi yake. Ikiwa mwanamke Myunani aliyekuwa na binti aliyepagagwa na mapepo angeponywa (Mariko 7:26-30). Ikiwa kibofu nche ya Yeriko angemwita Kristo kwa sauti, angebaki kibofu (Luka 18: 35-43). Mungu amesema kuwa kila mara tunaenda bila kwa sababu hatuulizi (Yakobo 4:2). Kwa njia nyingine maombi ni kama kushiriki injili na watu. Hatujui ni nani ataitikia ujumbe wa injili hadi pale tunapoishiriki. Kwa njia hiyo hiyo, hatuwezi kuyaona matunda ya maombi yakijibiwa hadi tuombe.

Ukusefu wa maombi yaonyesha ukosefu wa imani na ukosefu wa imani katika neno la Mungu. Tunaomba ili tuonyeshe imani yetu kwa Mungu, kuwa atatenda vile ameahidi katika neno lake na kubariki maisha yetu utele zaidi ya vile tumeuliza na kutumainia (Waefeso 3:20). Maombi ni njia ya kuona kazi ya Mungu katika maisha ya wengine. Kwa sababu ni njia yetu ya “kujitupa ndani” ya nguvu za Mungu, ni njia yetu ya kumshinda shetani na jeshi lake ambalo hatuna nguvu za kulishinda sisi wenyewe. Kwa hivyo Mungu anatupata kila mara mbele ya kiti chake cha enzi, kwa vile tuko nakuani mkuu mbinguni anayeweza jua yote amboyo tunayapitia (Waebrania 4:15-16). Tuko na ahadi yake kuwa maombi ya mwenye haki yatatenda mengi (Yakobo 5:16-18). Na Mungu atukuze jina lake katika maisha yetu tunapomwamini na kukuja kwake kila mara katika maombi.



JE! WAJUA KUWA MUNGU ANAKUPENDA?
 
1. MWENYEZI MUNGU ANAKUPENDA, NAYE ANATAKA KUKUPANGIA MPANGO WA AJABU KWA MAISHA YAKO.
UPENDO WA MUNGU
Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Yohana 3:16
MPANGO WA MUNGU KWAKO
Mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele. Yohana 10:10
Je, kwa nini watu wengi hawana uzima huo?
Ni kwa sababu . . .

2. MWANADAMU NI MWENYE DHAMBI. Dhambi zake zimemtenga na Mungu.Kwa hiyo hajui upendo na mpango wa Mungu kwa maisha yake.

MWANADAMU NI MWENYE DHAMBI
Kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.Warumi 3:23
Mungu alimwumba mwanadamu kwa kusudi la kushirikiana naye, lakini mwanadamu alikwenda kinyume cha mpango wa Mungu. Alichagua kumwasi Mungu badala ya kumtii. Kumwasi Mungu ni kufanya dhambi. Mtu anapoishi kinyume cha mapenzi ya Mungu anaendelea kuishi maisha ya dhambi.
MWANADAMU AMETENGANA NA MUNGU
Lakini maovu yenu yamewatenga ninyi na Mungu wenu. Isaya 59:2
Mungu Mtakatifu hana ushirika na dhambi. Kati yake na mwanadamu kuna ufa mkubwa wa dhambi. Mwanadamu hujaribu kumfikia Mungu kwa nija nyingi: dini, matendo mema, sala, n.k., lakini hizi zote hazitoshi. Mwanadamu bado ni mwenye dhambi.
Kuna njia moja tu ya kushirikiana na Mungu . .
3. YESU KRISTO NI NJIA YA PEKEE YA KUONDOA DHAMBI.
 Alikufa kwa ajili yetu ili tujue upendo na mpango wa Mungu kwa maisha yetu.
ALIKUFA ILI ATULETE KWA MUNGU
Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili yao wasio haki, ili atulete kwa Mungu.1 Petro 3:18
YESU YU HAI
Kristo alikufa kwa ojili ya dhambi zetu, kama yanenavyo maandiko; na ya kuwa alizikwa; na ya kuwa alitufuka siku ya tatu, kama yanenavyojil maandiko.1 Wakorintho 15:3,4
YESU NDIYE NJIA YA PEKEE
Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.Yohana 14:6

  
Mwanadamu peke yake hawezi kushirikiana na Mungu. Mungu alimtuma Yesu afe msalabani kwa ajili ya dhambi zetu na tena awe daraja kati yetu na Mungu ili atulete kwa Mungu.
Sasa kanuni ya nne itakuambia jinsi uwezavyo kumjua maishani mwako . . .

4. INAKUPASA KUMPOKEA YESU AWE MWOKOZI NA MTAWALA WAKO.
 Ndipo utajua upendo na mpango wa Mungu kwa maisha yako.
UNAMPOKEA KRISTO KWA IMANI
Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake.Yohana 1:12
Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani, ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu; wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu.Waefeso 2:8,9

INAKUPASA KUMKARIBISHA YESU, MAISHANI MWAKO
Tazama, nasimama milangoni, nabisha, mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake . . .
Kumpokea Yesu Kristo ni:
  1. Kujua wewe ni mwenye dhambi na kugeuka nafsi yako kwa Mungu na kutubu.
  2. Kumtegemea Mungu kwa kukusamehe kabisa.
  3. Kumkaribisha Yesu Kristo atawale maisha yako kwa imani, ili uwe kama anavyopenda.
Je, ni picha gani aliye mfano wa maisha yako?
Je, ni picha gani ambaye ungependa awe mfano wa maisha yako?
Yafuatayo ni maelezo ya jinsi uwezavyo kumpokea Kristo ndani ya maisha yako?

UNAWEZA KUMPOKEA KRISTO SASA
Mungu anaufahamu moyo wako. Yafuatayo katika sala hii yanaweza kukusaidia kumpokea Kristo ukiomba kwa moyo wa kweli.
Bwana Yesu Kristo, ninakuhitaji, mimi ni mwenye dhambi. Nimekubali kwamba nimejitawala maisha yangu mwenyewe, na kutengana nawe. Asante kwa kifo chako msalabani kwa ajili ya dhambi zangu na kwa kunisamehe zote. Sasa nageuka na kutubu. Bwana, nakuomba uingie ndani ya maisha yangu na kunitawala kabisa. Badili maisha yangu yawe kama upendavyo wewe. Amin.
Je, sala hii ni sawa na haja ya moyo wako?
Kama sala hii ni sawa na haja ya moyo wako, basi omba sasa na umkaribishe Kristo aingie maishani mwako.

YESU YUMO MAISHANI MWAKO
Sasa, je, umemkaribisha Yesu maishani mwako? Unajuaje?
Kwa hiyo yuko wapi sasa? Kumbuka Ufunuo 3:20.
Yesu alisema ataingia katika maisha yako. Je, si kweli?
Je, unajuaje kuwa Mungu amesikia ombi lako? Mungu ameahidi kwanba lo lote tuombalo na kuamini litatendeka.
ALIYE NA YESU, ANAO UZIMA WA MILELE
Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele na uzima huu umo katika Mwana. Yeye aliye naye Mwana, anao huo uzima; asiye naye Mwana wa Mungu hana huo uzima. Nimewaandikia ninyi mambo hayo, ili mjue ya kuwa mna uzima wa milele, ninyi mnaoliamini jina la Mwana wa Mungu. 1 Yohana 5:11-13
Umshukuru Mungu kila siku kwamba Yesu anaishi katika maisha yako.
Uwe na hakika kwamba hatakuacha kabisa. (Mathayo 28:20). Amekupa uzima wa milele.
  
USIYATEGEMEE MAWAZO YA MOYO WAKO.
Unaweza kujisikia leo unalfuraha kisha kesho ukawa na huzuni. Kwa vyovyote utakavyojisikia Yesu Kristo habadiliki maishani mwako. Waebrania 13:8.
  • Ukweli wa Mungu ndio wenye uwezo wa kutuongoza.
  • Tunaunganishwa na uwezo wa ukweli kwa imani.
  • Tunapotii ukweli, hali ya kujisikia ya moyo (maoni) huongozwa vyema.
  • Tunamtegea Mungu na ukweli wake wala sio hali ya kujisikia ya moyo.
Tukifanya dhambi tunatubu na yeye anatusamehe.
Basi, usitegemee mawazo yako, bali utegemee ukweli wa Neno la Mungu kwa imani.
KWA KUWA SASA UMEMPOKEA YESU
Tangu ulipompokea Kristo mabadiliko mengi yametokea.
  1. Yesu ameingia katika maisha yako. (Ufunuo 3:20)
  2. Umesamehewa dhambi zako. (Wakolosai 1:14)
  3. Umefanyika kuwa mwana wa Mungu. (Yohana 1:12)
  4. Utazidi kujua makusudi ya Mungu kwa maisha yako. (2 Wakorintho 5:14,15,17)
Je, unafikiri kuna jambo lililo bora kuliko kumpokea Yesu katika maisha yako?
Basi, labda ungependa kumshukuru Mungu sasa kwa vile alivyokurehemu.
Tunathibitisha imani yetu tunapomshukuru Mungu kwa maombi.
Tuombe tukiwa huru.

Na sasa je?
JINSI YA KUKUA KIROHO
Kama mtoto mchanga unahitaji kukua
Utaendelea vizuri katika maisha ya kiroho ukiyafuata mashauri yafuatayo kila siku:
  1. Zungumza na Mungu kwa maombi (Yohana 15:7)
  2. Soma Neno la Mungu (Matendo 17:11)
  3. Uwe mwaminifu kwa Mungu (Yohana 14:21)
  4. Mshuhudie Kristo kwa matendo yako na maneno yako (Mathayo 4:19 na Yohana 15:8)
  5. Umtumaini Mungu kwa kila jambo katika maisha yako (1 Petro 5:7)
  6. Umruhusu Roho Mtakatifu akutawale (Wagalatia 5:16-18 na Matendo 1:8)
NI MUHIMU KWA WAKRISTO KUSHIRIKIANA
Biblia inatuambia kukusanyika pamoja (Waebrania 10:25)
Ebu, tutumie mfano wa moto. Kuni nyingi zikirundikwa pamoja zinawaka vizuri sana, lakini ukiuondoa ukuni mmoja na kuuweka peke yake utapoa. Vile vile wewe haifai kuishi maisha ya kikristo peke yako.
Ukishirikiana na watu wengine ambao wamempokea Yesu kuwa Mwokozi wao utazidi kuwa na moto wa imani.
Uhudhurie kanisa ambapo watu wanaiamini Biblia kuwa ni kweli na Yesu anatukuzwa.